Katika blogu hii, tutachunguza njia mbalimbali za kuimarisha ufahamu wetu wa Biblia. Tutajadili mbinu za kusoma Biblia kwa ufanisi, vidokezo vya kukariri maandiko matakatifu, na mikakati ya kutumia somo la Biblia katika maisha yetu ya kila siku. Iwe wewe ni mtaalam wa Biblia mzoefu au unaanza tu safari yako ya imani, "Jifunze Biblia Zaidi" ni rasilimali kamili ya kukusaidia kuongeza ufahamu wako wa Maandiko Matakatifu na kumkaribia Mungu zaidi.

2.IFUATAYO NDIYO NJIA YA KUMTAMBUA NABII WA KWELI NA NABII WA UONGO.

1.   IFUATAYO NDIYO NJIA YA KUMTAMBUA NABII WA KWELI NA NABII WA UONGO.

SOMO:MIUJIZA INAENDELEA................................


Na katika hili twajua ya kuwa tumemjua yeye ikiwa tunashika amri zake. Yeye asemaye, nimemjua, wala hazishiki amri zake, ni muongo, wala kweli haimo ndani yake” 1YOHANA 2:3-4

“kwa maana watu hawa ni watu waasi, watoto wasemao uongo, watoto wasiotaka kuisikia sheria ya BWANA”ISAYA 30: 9

          Kipimo cha kumtambua nabii wa kweli na nabii wa uongo kiko katika Biblia yenyewe, usiulize mchungaji wako, usiulize wazazi wako, wala mke au mume wako,usiulize mwanao.Na kipimo hicho ni ikiwa anazishika amri. Na kama anadai kumjua MUNGU na huku hazishiki amri ndiye nabii wa uongo;wala kweli (neno la Mungu) halimo ndani yake (Yohana17:17) Kwa maana wasio taka kuitii sheria ya MUNGU ni waasi, na wanamafundisho ya uongo. Hata maombi yao ni udanganyifu tu maana MUNGU ameangiza ifuatavyo juu ya maombi;

“Na lolote tuombalo tutalipokea kwake, kwakuwa twazishika amri zake; na kuyatenda yapendezayo machoni pake”1YOHANA 3:22

           Mpenzi msomaji ili kumjua nabii wa uongo Biblia hapa inachofundisha ni kuwa wanakataa amri kumi za MUNGU.Na mojawapo ya amri kumi ni amri ya nne, yaani amri ya sabato, na huo ndio mpango wa shetani leo kuwafanya watu wawe wanasali lakini wanavunja amri angalau moja tu, basi huwa makusudi yake yametimia.Maana katika hesabu ya mbinguni amri kumi ukitoa amri moja jawabu ni sifuri.Divyo neno la MUNGU linavyotufundisha katika kitabu cha Yakobo;Neno linasema;

“Maana mtu awaye yote atakayeshika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja (amri moja) amekosa juu ya yote. Kwa maana yeye aliyesema, usizini, pia alisema, usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria”YAKOBO 2;10-11

 

Hiki ndicho kipimo

1.   Nabiiwa kweli anashika amri kumi

2.   Nabii wa uongo anakataa amri kumi

Uchaguzi ni wako utaenda wapi? MUNGU anawatumishi wanashika amri.

Shetani naye anawatumishi hawataki amri, ila wanafanya miujiza, na wakiwa na majina makubwa makubwa.Mara utasikia matangazo huyu anayekuja ni nabii na mtume. Lakini wao wenyewe hawakubaliani, kila mtu anakanisa lake.Kwanini hawapatani, kwanini hawakubaliani, wakati mitume na manabii wa MUNGU hawakupingana?Kupitia manabii hawa injili makanisani imebadilika;

·         Kila kanisa njoo uponywe

·         Kilakanisa njoo utajirike

·         Kila kanisa njoo upandishwe cheo

·         Kila kanisa njoo upate mchumba

Manabii wa uongo wanaibada,wanasali, wanamakanisa na wangeitumia biblia, na wengetumia jina la Yesu.Lakini wakiwa na lengo la kupoteza hata wateule.

“Umizimu sasa unababdilisha mfumo wake, ukiwa umeficha baadhi ya sehemu zake muhimu zinazochukiza, sasa umejivika vazi la Kikristo …. Wakati zamani ulimkana Kristo na Biblia, sasa unakiri kukubali vyote viwili” (Biblia na Ukristo) E.G White – Dhiki kuu uk,61:1

 

3.   KIAPO CHA SHETANI

“Nawe ulisema moyoni mwako, nitapanda mpaka mbinguni, nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za MUNGU; nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, katika pande za mwisho za kaskazini.Nitapaa kupita vimo vya mawingu, nitafanana na yeye aliye juu. Lakini utashushwa mpaka kuzimu; mpaka pande za mwisho za shimo. Wao wakuonao watakukazia macho, watakuangalia sana, wakisema je! huyu ndiye aliyeitetemesha dunia, huyu ndiye aliyetikisa falme; aliyeufanya ulimwengu ukiwa akaipindua miji yake; asiyewafungua wafungwa wake waende kwao?”ISAYA 14;13

 

 

Hiki ndicho kiapo cha shetani; ingawa na angamizo lake linatajwa hapo hapo. Aliapa kuwa angefanana na yeye aliye juu.

1.   Aliye juu anakanisa – shetani naye ana makanisa

2.   Aliye juu anaabudiwa – shetani naye anaabudiwa

3.   Aliye juu anamanabii – shetani naye ana manabii

4.   Aliye juu ana mitume – shetani naye ana mitume

Ila cha ajabu watumishi wa shetani wangefanyaibada, miujiza, siyo kwa jina la shetani, bali kwa jina Yesu; ndipo ulimwengu ungewapokea na kuwaamini. Ndugu msomaji katika jambo hili umepona?

“Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea, wachungaji wao wamewapoteza; wamewapotosha milimani;(makanisani) wamekwenda toka mlima hata mlima (kanisa hadi kanisa)wamesahau mahali pao pa kupumzika”.                 YEREMIA 50: 6

Mpaka leo ni watu wengi wanaohama kanisa hadi kanisa wakitafuta miujiza, wengine wakitafuta ukweli; sababu ya kukoseshwa na wachungaji. Na watu wamesahau mahali pao pa kuabudu yaani kwa wanao shika amri.

“Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu wagonjwa, nao watapata afya”MARKO 16:17

          Shetani akalidaka hilo maana aliazimu kufanana na yeye aliye juu. Swali,je, watumishi wa shetani wanao uwezo wa kufanya miujiza? Ndio; mtumishi wa Mungu Paulo anajibu swali hili;

“Maana watu kama hao ni mitume wa uongo, watendao kazi kwa hila, wanaojigeuza wawe mfano wa mitume wa Kristo.Wala si ajabu.Maana shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumushi wa haki ambao mwisho wao utakuwa sawasawana kazi zao’’2 KORINTHO 11;13-15.




 Mpendwa msomaji endelea kufuatilia makala hii na Mungu akubariki AMINAAA!!!!!!
                               ITAENDELEA....
Share:

Popular Posts

Lebo

Recent Posts

Pages